Taasisi ya Elimu ya kitanzania "NLab" Imeshinda TUZO nchini GHANA

 Kutokana na mashindano yaliyo fanyika nchini GHANA yakihusisha watu, makampuni na Taasisi zilizo anzishwa na vijana mbali mbali katika kutatua changamoto zinazo likumba bala la Africa Taasisi ya elimu ya NLab Innovation Academy ilijinyakulia Tuzo katika kipengele cha mtoa elimu mwenye kuongeza thamani.

Tuzo hizo zilitolewa tarehe 9 mwezi wa 11 mwaka 2018,  zilipokelewa na Gloria Clement ambaye ni Mshauri wa mambo ya Biashara, Uwekezaji na Mafunzo katika chuo hicho ambaye.  Mara baada ya kupokea Tuzo hiyo, Gloria alipata nafasi ya Kuzungumza na kuweza kuweka bayana mipangoi ambayo chuo hicho kimejiwekea katika kutatua changamoto za ajira huku kikiongeza thamani katika mafunzo wanayo yatoa ili yaweze kumsaidia mwanafunzi husika baada ya kupokea mafunzo hayo.

Picha ikionesha jopo la wazungumzaji katika "Summit" ya vijana iliyo fanyika nchini ghana mjini Accra.

Picha ikionesha washindi walio pokea tuzo. 


Gloria Clement  wapili kutoka kulia mwenye Top nyeusi na Suruali ya kitenge akiwa na washindi baadhi

Nje Ya Box

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi