Daktari Mbaroni Kwa kulazimisha kumtoa mtu mimba


 Huenda alifanya kwa kumsaidia lakini msaada wake umemgeuka na kuwa hatia, Dk. Thomas A. Pfeiffer, amefikishwa Mahakamani kutokana na kufanya kosa la kumlazimisha mwanamke mmoja kunywa dawa za kutoa ujauzito.

Dokta huyo wa New York amekutwa na hatia, anatakiwa kujibu mashtaka matatu ambayo yametokana na kumlazimisha mwanamke mmoja kunywa dawa za kutoa ujauzito, amefikishwa Mahakamani kusomewa mashtaka kisha kurudishwa jela na dhamana yake ni dola 50,000.

Daktari kaingia kwenye hatia hiyo baada ya upelelezi kubaini kwamba anahusika na kitendo hicho ambapo mwanamke aliyetumia dawa hizo alipata majeraha sehemu za kooni na mdomoni.

Nje Ya Box

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi